Leba Dei Bila Pesa: Rais Ruto awaacha wafanyikazi wa Kenya bila pesa
Wafanyikazi wa Kenya walikosa cha kutabasamu hii leo huku taifa likiadhimisha sikukuu ya Leba Dei. Maadhimisho ya mwaka huu yakiwaacha wafanyakazi mikono mitupu huku serikali ikidinda kuongeza mapato ya vibarua. Mbali na hayo serikali imejitenga kabisa na kashfa ya kuwalaghai wakenya kuhusu kazi ughaibuni na badala yake ikisifia nafasi zaidi za kazi. Jimmy Mbogoh anaarifu.