Serikali ya kaunti yaendelea kuwafurusha wadeni
Maelfu ya wakazi jijini Nairobi wanaoishi katika nyumba zinazomilikiwa na serikali ya kaunti ya Nairobi wanaishi kwa hofu kufuatia hatua ya serikali ya kaunti kuanza kuwafurusha wale wanaodai wana madeni ya kodi. Zoezi hilo ambalo limefanyika katika mitaa ya Jamhuri, Kariokor na Woodley limezua tetesi kutoka kwa wakazi ambao sasa wanataka mazungumzo na gavana johnson sakaja ili kupata suluhu